Posted by admin on 2025-10-06 12:33:42 |
Share: Facebook | Twitter | Whatsapp | Linkedin Visits: 40
Kaulimbiu ya mafunzo siku ya maadhimisho: “Mchango wa Wazee katika Kuimarisha
Maadili, Ustawi na Haki za Jamii”
Wazee ni nguzo ya maadili, hazina ya hekima, na washiriki hai
wa maendeleo. Ustawi wao ni ustawi wa familia, jamii na taifa. Wanastahili
heshima, haki, na ushiriki kamili katika maisha ya kijamii na kitaifa.
1.
Wazee kama nguzo
ya maadili
i.
Kurithisha maadili mema kwa vizazi vipya
kupitia simulizi, ushauri na mfano wa maisha.
ii.
Kudumisha mshikamano wa kifamilia na
kijamii.
iii.
Kuongoza jamii katika maadili ya kiroho na
kijamii.
2.
Ustawi wa wazee
ni ustawi wa jamii
i.
Upatikanaji wa huduma bora za afya na
lishe.
ii.
Ushirikiano wa kijamii ili kuepuka upweke.
iii.
Kujenga urithi wa amani, mshikamano na
maridhiano kati ya vizazi.
3.
Haki za msingi
za wazee
i.
Heshima na utu, bila kudharauliwa au
kunyanyaswa.
ii.
Haki ya huduma za afya, hifadhi ya jamii,
na kushiriki katika maamuzi.
iii.
Kulindwa dhidi ya ukatili na kudhulumiwa
mali au urithi wao.
“Kuhakikisha wazee wanashiriki katika
uchaguzi kwa ustawi wao”
i.
Kura ni sauti ya mzee.
ii.
Ustawi wa mzee unategemea viongozi bora.
iii.
Mzee ni mshiriki, si mtazamaji.
iv.
Ushiriki hujenga heshima na utu wa mzee.
v.
Ustawi wa pamoja ni ustawi wa familia,
jamii na taifa.
i.
Walinzi wa mila na desturi njema.
ii.
Walezi wa familia na jamii.
iii.
Viongozi wa maadili na tabia njema.
iv.
Waamuzi na wapatanishi wa migogoro.
v.
Mabalozi wa mabadiliko katika kupinga
ukatili wa kijinsia.
MATOKEO YA MAADHIMISHO YA 2025
1.
Mahudhurio
i.
Kata ya Kwala tulifaya maadhimisho siku ya
Jumatano Oktoba 1, 2025
ii.
Wazee 314 kuanzia miaka 55 walihudhuria na
kushiriki mafunzo kama sehemu ya maadhimisho
iii.
Kata ya Miono tulifanya maadhimisho siku
ya Alhamisi Oktoba 2, 2025
iv.
Wazee 109 kuanzia miaka 60 walihudhuria na
kushiriki mafunzo kama sehemu ya maadhimisho
2.
Ombi la Wazee kwa Taifa Kupitia Equip for
Change
i.
Wazee wanaomba kupewa Bima ya Afya ili
kusaidia upatikanaji wa huduma za afya kwa unafuu kwao.
ii.
Wazee wanaojishughulisha na kilimo
waliomba kusaidiwa mashine inayoweza kusaidia na kurahisha kazi ya kilimo
kuanzia kulima, kupanda, kupalilia na kuvuna.
iii.
Wazee ambao bado wana nguvu na
wanajishughulisha kijasiriamali waliomba kuingizwa kwenye mpango wa kuewa
mikopo kama na halmashauri zao kama ilivyo kwa kundi la vijana na wanawake.
iv.
Wazee waliomba kupewa majiko ya Gesi
asilia ili kujipatia nishati mbadala kuepuka matumizi ya kuni na mkaa ili
kulinda afya zao dhidi ya moshi.
v.
Wazee waliomba angalau kila baada ya mizei
mitatu wawe wanakutanishwa na kupewa mafunzo mbalimbali kama njia ya kupunguza
msongo wa mawazo na kuchangamsha akili zao na mbinu ya kulinda afya ya miili
yao na afya ya akili.
vi.
Wazee waliomba Serikali ijitahidi kukabili
janga la ukosevu wa ajira kwa vijana ili vijana waliosoma waweze kuajiriwa na
kukidhi mahitaji ya maisha yao na maisha ya wazee wao waliowasomesha
vii.
Wazee waliomba Kamari za aina zote zipigwe
marufuku maana zimeua moyo wa vijana kujiajiri na kushiriki shughuli za kilimo,
uvuvi na ufugaji, mambo ambayo yana tija katika kukuza uchumi ya familia na
taifa pia.
viii.
Wazee walijipa jukumu la kuacha na kukemea
tabia zote zinazochochea vitenda vya ukatili wa kijinsia hasa ndoa na mimba za
utotoni.
ix.
Wazee waliomba Serikali iwe makini sana
inapoajiri walimu kwa sababu walimu wengi sasa wameanza kuonesha tabia
zinazochangia kuongeza sana kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto
wa kike mashuleni.
x.
Wazee waliomba kila inapowezekana wawe
wanapatiwa posho ya kujikimu
🌿 Hitimisho:
Wazee ni daraja kati ya vizazi. Kuwaheshimu na kuwatambua si tu kuendeleza
urithi wa hekima, bali pia ni msingi wa kujenga jamii yenye mshikamano, heshima
na ustawi wa pamoja.