SAFARI YA UHURU WA KIFEDHA – KIZAZI CHA WANAFUNZI 12 WAMEHITIMU!

SAFARI YA UHURU WA KIFEDHA KIZAZI CHA WANAFUNZI 12 WAMEHITIMU!

Posted by admin on 2025-10-25 14:29:39 |

Share: Facebook | Twitter | Whatsapp | Linkedin Visits: 18


SAFARI YA UHURU WA KIFEDHA – KIZAZI CHA WANAFUNZI 12 WAMEHITIMU!

Mnamo tarehe 16 Oktoba 2025, wanafunzi 12 (wavulana 6 na wasichana 6) walihitimu mafunzo ya Safari ya Uhuru wa Kifedha yaliyoandaliwa na Equip for Change. Mafunzo haya yaliyofanyika Dar es Salaam, yalitumia mwongozo wa African Money Map unaotokana na mafundisho ya Crown Financial Ministries, unaosaidia watu kutembea katika safari ya kiroho na kiuchumi kuelekea uhuru wa kifedha wa kweli.

Kupitia somo hili, washiriki walijifunza kanuni za Biblia kuhusu:

l  Umiliki na usimamizi (stewardship) — kutambua kuwa Mungu ndiye mmiliki wa yote; sisi ni wasimamizi wake.

l  Kazi kwa uaminifu na nidhamu — kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo wote kama kwa Bwana.

l  Udhibiti wa matumizi, kulipa madeni, kuokoa, na kutoa kwa ukarimu.

l  Kujenga uhusiano mzuri na Mungu, familia, na jamii kupitia uaminifu na uadilifu.

Washiriki walihimizwa kutekeleza walichojifunza nyumbani kwa kuandaa bajeti, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, na kuanza kuweka akiba na kuiwekeza kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Tunaamini kwamba haya ni mavuno mapya ya maisha yaliyobadilishwa — safari ya kutoka katika utumwa wa madeni na matumizi mabaya ya fedha kwenda kwenye uhuru wa kifedha unaomtukuza Mungu.

 

Mafunzo yaliendeshwa na Mkufunzi CFE, Rev. John Wambura


Leave a Comment: